23.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Avamia chuo kikuu, aua sita

MWANAUME aliyeingia Chuo Kuu mjini Perm, Urusi, amewaua kwa kuwapiga risasi watu sita.


Mtu huyo aliingia chuoni hapo asubuhi ya leo na kisha kuanza kupifa risasi, ambapo wanafunzi na waalimu wao walilazimika kujifungia vyumbani, wengine wakiruka kupitia madirishani.


Polisi waliothibitisha tukio hilo wamedai kumjeruhi muhusika aliyetajwa kuwa ni mwanafunzi wa chuoni hapo, wakiongeza kuwa wanafunzi zaidi ya 20 walijeruhiwa.

Aidha, vyanzo vingine vya habari vimeripoti kuwa watu nane walifariki. Akizungumzia kilichotokea, mmoja wa wanafunzi, Semyon Karyakin, amesema: “Tulikuwa na wanafunzi kama 60 darasani. Tulifunga mlango na kuuwekea viti,”

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles