29.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 18, 2024

Contact us: [email protected]

‘ASPIRIN NI HATARI KWA WENYE UMRI MKUBWA’

Pretoria, Afrika Kusini

WATU wenye umri wa zaidi ya miaka 75 ambao hutumia Aspirin baada ya kupatwa kiharusi au maradhi ya moyo, wako hatarini kupata matatizo ya kuvuja damu tumboni, kwa mujibu wa Shirika la Utafiti wa Utabibu la Lancet.

Wanasayansi wanasema  kupunguza athari hizo, watu wenye umri mkubwa wanapaswa kumeza dawa za kuzuia maradhi ya tumboni (PPI).

Lakini wamesisitiza kuwa Aspirin ina faida muhimu kama vile kuzuia maradhi ya moyo.

Utafiti wa utabibu  Uingereza umeonyesha  kwamba kutumia vidonge vya   Aspirin kuna athari kubwa zaidi kuliko ilivyodhaniwa   awali, hususan kwa watu wenye umri mkubwa.

Dawa hiyo ambayo inatumiwa kwa kiwango kikubwa kuzuia mshtuko wa moyo na maradhi ya kiharusi imehusishwa kwa siku nyingi kusababisha matatizo ya kuvuja damu   tumboni.

Wataalamu hao wametahadharisha kuwa kusimamisha ghafla matumizi ya Aspirin kunaweza kuleta madhara, hivyo mtu yeyote anashauriwa kupata ushauri wa daktari ikiwa anatakiwa kubadili dawa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles