30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Andengenye: Tumefurahishwa na kampeni ya TRA ya mlango kwa mlango

MWANDISHI WETU-KIGOMA

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Thobias Andengenye amesema amefurahishwa na kampeni ya elimu ya kodi ya mlango kwa mlango inayoendeshwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoani Kigoma na kwamba wafanyabiashara wanaohofia kunyang’anywa faida zao na wanatakiwa kutumia nafasi hiyo kuhoji maswali na kupata elimu.

Akizungumza baada ya kutembelewa na maafisa wa TRA kutoka makao makuu waliofika mkoani hapa kwaajili ya kuendesha kampeni ya elimu ya kodi mlango kwa mlango, Andengenye amesema huu ni wakati wa wafanyabiashara wa kukidhi kiu yao ya maswali kuhusu kodi pamoja na changamoto wanazokutana nazo ili waweze kutatuliwa na maofisa hawa wa TRA ambao wamekuja kukusanya pesa ya serikali inayotokana na biashara wanazofanya.

Amesema kampeni hiyo itawawezesha kujua kuwa pesa zinazokusanywa sio za TRA na kwamba ni za serikali ambazo zitamgusa kila mmoja kutokana na miradi ambayo inatekelezwa na serikali.

“Nawashauri wafanyabiashara watoe ushirikiano kwa maofisa wetu na sehemu ambayo watakuwa hawajaelewa wanatakiwa kuuliza ili kuelekezwa na kwamba huu ni wakati wao na kwamba lengo ni kujenga urafiki baina ya TRA na walipakodi,” anasema Andengenye.

Naye meneja wa TRA mkoa wa Kigoma, Jackob Mtemang’ombe  anasema kuwa mkakati wa TRAni kuhakikisha inaeneza elimu ya kodi kwa kila mwananchi kwa urahisi na kwamba kampeni hii ya mlango kwa mlango ni nzuri kutokana na kuwa elimu itawafikia kwa urahisi kutokana na kuwa watafikiwa katika maeneo yao.

Anasema ni vingumu kwa walipakodi kuacha biashara zao na kuhudhuria semina za kodi hivyo TRA imeamua kuwafata ili kuwarahisishia ikiwa ni pamoja na kuona mazingira wanayofanyia biashara zao na changamoto wanazokutana nazo.

“Ni rahisi kumuelimisha mlipakodi akiwa katika eneo lake la biashara ukilinganisha akiwa mbali na kwamba baada ya kuwaelimisha ndipo tutaanza kufuata sheria kutokana na kuwa watakuwa wameshapata uelewa,” anasema Mtemang’ombe.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles