24.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

Amber Rose ataka mtoto wa pili na Wiz Khalifa

Amber RoseNEW YORK, MAREKANI

MWANAMITINDO maarufu  nchini Marekani, Amber Rose, ameweka wazi kuwa anataka mtoto wa pili ili mtoto wake wa kwanza apate mdogo wake.

Mrembo huyo alifanikiwa kupata mtoto na rapa, Wiz Khalifa, mtoto wao kwa sasa ana miaka mitatu anajulikana kwa jina la Sebastian.

Hata hivyo, mrembo huyo anadai kuwa atakuwa na furaha zaidi kama atafanikiwa kuzaa na baba mtoto wake, Wiz Khalifa.

“Nipo tayari kupata mtoto wa pili kwa ajili ya mwanangu awe na mdogo wake wa kike au wa kiume azidi kuwa na furaha, ninaamini ninaweza kufanya hivyo lakini natamani nizae tena na Wiz Khalifa,

“Bado nina uhusiano wa karibu lakini si wa kimapenzi, natarajia kumwambia kama atakuwa tayari anizalishe mtoto wa pili,” alisema Amber Rose.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles