27.1 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Aliyedai kuporwa fedha na Lukuvi aachiwa huru

PATRICIA KIMELEMETA
Mahakama ya Wilaya ya Ilala imemuachia huru, Mohamed Kiluwa (50) aliyekuwa akikabiliwa na shtaka la kutoa rushwa ya Sh milioni 90 kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi kwa sababu ushahidi wa mashtaka ulikuwa wa hisia.

Akisoma hukumu hiyo leo Jumatatu Desemba 24, Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama hiyo Samuel Obas amesema ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka haukuwa na mashiko kwa sababu umeshindwa kuthibitisha kosa.

Amesema kutokana na hali hiyo, mahakama hiyo imemuachia huru na kuamuru fedha zake ambazo ni Sh milioni 90 arudishiwe.
Hata hivyo, ameruhusu upande wa jamhuri kukata rufaa kama hawajaridhika na uamuzi huo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles