27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

ALIKIBA KUTUMBUIZA TAMASHA LA ONE AFRICA MAREKANI

TAMASHA la muziki la watu kutoka Afrika wanaoishi nchini Marekani, One Africa Music Festival 2017, linatarajia kufanyika leo kwenye uwanja wa Amphitheatre Coney, Brooklyn New York nchini humo huku msanii Ali Kiba akitumbuiza sambamba na wasanii wengine wa Afrika.

Staa huyo ambaye hivi karibuni anatarajia kuachia ngoma yake mpya inayoitwa Kipusa, atatumbuiza jukwaa moja na mastaa wa Afrika kama kundi la P Square, Cassper Nyovest, Tiwa Savage, 2 Face na wengineo.

Mastaa wengine wa muziki watakaotumbuiza kwenye tamasha hilo la One Africa linalofanyika kila mwaka ni Tekno, Mr Flavour, Victoria Kimani, Davido, Banky W na Timaya.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles