31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Akutwa na kilo moja ya misumari tumboni

MWANAUME raia wa Lithuania amefanyiwa upasuaji na kukutwa na kilogramu zaidi ya moja ya misumari, nati na visu kwenye tumbo lake.

Upasuaji huo uliochukua saa tatu ulifanyika katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Klaipeda na madaktari wamekiri kuwa hilo ni jambo la ajabu zaidi kuwahi kukutana nalo katika shughuli zao.

Kwa mujibu wa kile kilichoelezwa na madaktari, mwanaume huyo alifikishwa hospitali kwa gari la wagonjwa na kilichokuwa kikimsumbua ni maumivu makali ya tumbo.

Wakizungumzia sababu ya vifaa hivyo kukutwa mwilini, madaktari wamesema jamaa alikuwa akimeza kimoja kimoja kila siku, akifanya hivyo ndani ya mwezi mmoja ili tu asahau tabia yake ya kunywa pombe.Juu ya hali yake, jamaa anaendelea vizuri, ingawa bado madaktari wa Hospitali hiyo wanaendelea kuifuatilia hali yake

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles