31.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Wachezaji Simba, Yanga na Azam wachanjwa

Na WINFRIDA MTOI, Mtanzania Digital

Wachezaji wa timu za Simba, Yanga na Azam leo wamepata chanjo ya kinga ya ugonjwa wa Corona katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKC) iliyopo Hospital ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam.

Wachezaji hao pamoja na viongozi wa benchi la ufundi na klabu, kabla ya kupata chanjo, walipewa semina fupi na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Prof. Mohamed Janabi.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano wa Yanga, Hersi Said, amesema kitendo cha kupata chanjo hiyo ni harakati za kuwalinda wachezaji wao ukizingatia wanatarajia kwenda kushiriki michuano ya Kimataifa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles