25.2 C
Dar es Salaam
Friday, October 18, 2024

Contact us: [email protected]

10 wapunguzwa BSS

BSSWASHIRIKI 10 waliokuwa katika shindano la kusaka vipaji la Bongo Stars Search 2015 (BSS), wameaga rasmi usiku wa kuamkia leo.

Washiriki hao walioagwa ni Evance Ernest, Khalid Iddy, Jabu Msangi, Mango Joshua na Jerome Benedicto kutokea Dar es Salaam.

Wengine ni Elisia Moshi, Christina Mbonde wa Mbeya na Ally Kala wa Mwanza na Gervas Miovela wa Arusha.

Majaji wa shindano hilo ambao ni Ritha Paulsen, Master Jay na Salama Jabir, ndio waliohusika katika mchujo huo.

“Kwa kuwa mwisho wa siku atakuja kupatikana mmoja, sisi kazi yetu ilikuwa ni kuwachuja kutoka 30 hadi 20 na kisha inakuja kubakia kazi ya wananchi kuchagua kwa kuwapigia kura washiriki watakaowataka washinde,” alisema Ritha Paulsen.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
590,000SubscribersSubscribe

Latest Articles