27.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 18, 2024

Contact us: [email protected]

Wakazi wa Bukoba watumia mitubwi


Ramadhan Hassan,Dodoma

Mbunge  wa Bukoba Mjini,Wilfred Lwakatare (Chadema)  amesema kutokana na mafuriko yanayotokea katika Mji huo  maji yamesambaa  kiasi cha kupelekea  watu kutoka katika mtaa mmoja kwenda  mwingine kwa  kutumia mtumbwi.

Akiomba mwongozo bungeni leo   Mei 28,Lwakatare amesema  hali ni tete katika eneo la Bukoba kufuatia mvua ambazo zimeendelea kunyesha kuathiri wakazi wa maeneo hayo.

“Kufuatia mvua ambazo zimeendelea kunyesha hivi sasa kuna mafuriko makubwa sana katika Manispaa ya Bukoba ambapo mtu mmoja mbaye ni mtoto amefariki na nyumba zaidi ya 75 zimepata maafa makubwa.

“pia maji yale yamesambaa ndani ya mji kiasi cha kupelekea  watu kutoka katika mtaa kwenda mtaa mwingine kutumia mtumbwi.

“Kwa hiyo naleta hoja Mheshimiwa Mwenyekiti kwamba unikubalie hoja hii ili iweze kujadiliwa kwa maslahi  mapana ya watu wa Bukoba ili hali inayoendelea ambayo imewaweka katika wasiwasi na kufikiria labda ule Mji   umelaaniwa kutokana na matukio ambayo yanaendelea kutokea,”amesema Lwakatare

Akijibu,mwongozo huo,Mwenyekiti wa Bunge,Najma Giga amesema : “Suala la Rwekatare hatuwezi kulijalidi kwa sababu suala la mvua linatokea maeneo mengi nchini ni  jukumu la Serikali kulifanyia kazi jambo hilo.  

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles