24.7 C
Dar es Salaam
Tuesday, March 19, 2024

Contact us: [email protected]

Yanga yatangaza kamati mpya ya Uchaguzi

Lulu Ringo, Dar es Salaam

Klabu ya Yanga imeunda kamati mpya ya uchaguzi mdogo ambayo itashirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), katika uchaguzi kwa nafasi za viongozi zilizoachwa wazi baada ya wengine kujiuzulu.

Viongozi waliojiuzulu nafasi zao katika klabu hiyo ni  Mwenyekiti Yusuph Manji, Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga, wajumbe Hashimu Adballah, Salum Nkemi, Omary Said na Ayoub Nyenzi.

Awali uchaguzi huo ulipangwa kufanyika Januari 13 mwaka huu, lakini ulihairishwa baada ya baadhi ya wanachama kwenda kuweka pingamizi mahakamani.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya klabu hiyo, leo Februari 21, Makamu mwenyekiti wa Yanga, Siza Lyimo, amesema tayari uongozi umeshachagua kamati ya uchaguzi ambao itaongozwa na  Venance Mwamoto Mbunge wa Kilolo Iringa, na katibu wake Seif Gulamali Mbunge wa Igunga, Dastan  Kitandula Mbunge wa Mkinga  na  Saidi Mtanda Mkuu wa Wilaya na Nkasi.

“Yanga kwa kushirikiana na TFF tayari tumepata majina manne mengine ya kamati ya uchaguzi, kwa kuwa mwanzo tulipeleka majina  lakini yalipoteza sifa hivyo tukaunda kamati nyingine, naamini uchaguzi huo kwa kushirikiana na wanayanga utakwenda vizuri,” amesema Siza

Aidha Mkuu wa Kitengo cha Habari wa klabu hiyo, Dismas Ten, amesema timu ya Yanga inatarajia kuondoka kesho kwenda Mkoani Lindi kwa ajili ya mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam dhidi ya Namungo FC katika hatua ya 16 Bora, mchezo utakaochezwa Jumapili Februari 24, Uwanja wa Majaliwa mkoani wa humo.

Dismas amesema ratiba bado ya michezo mbalimbali ya klabu yao bado haijakaa vizuri ukizingatia na umbali wa sehemu wanazoenda kucheza kwa kuwa hali hiyo imekuwa changamoto kubwa katika timu.

“Tumetoka kucheza Mwanza, tumerudi tunaenda kucheza na Namungo FC , baada ya hapo tutaenda tena Mwanza kucheza dhidi ya Allience na timu itarudi tena Dar es Salaam kucheza na KMC na baada ya hapo itelekea tena Iringa kucheza na Lipuli FC, hivyo hali hii inaweza kuleta changamoto ya timu kutofanya vizuri  hivyo tunaomba bodi ya ligi  kutazama kwa umakini suala hili,” amesema Dismas.

Katika hatua nyingine Mtaribu wa klabu hiyo, Hafidhi Salehe, ametaja kiasi cha  fedha ambacho kimepatikana hadi kufikia leo Februari 21 tangu kuanzishwa kwa mchakato wa kuchangia timu hiyo na Kocha Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera mwanzoni mwa Februari mwaka huu katika miamala ya M Pesa, Tigo Pesa na Benki ya CRDB.

 “Wakati tunaanza mchakato huu  tuliwaahidi wadau kuwa tutakuwa tunatoa mrejesho kila wiki lakini kutokana na ratiba kubana hatukuweza kufanya hivyo, mpaka sasa tumekusanya zaidi ya Sh milioni 21 kutoka kwenye Tigo Pesa, M pesa na akaunti ya benki ya CRDB.

“ Tunashukuru kwa wadau ambao wameendelea kutuchangia lakini bado kiasi hiki cha fedha hakitoshi kutokana na mahitaji ambayo kocha alisema anahitaji kuyatimiza hivyo tunaomba muendelee kujitolea kuisaidia timu,” ame sema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
584,000SubscribersSubscribe

Latest Articles