27.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 18, 2024

Contact us: [email protected]

Wenye magari kicheko bei ya mafuta yashuka

Na MWANDISHI WETU -DAR ES SALAAM

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA imetangaza bei kikomo   ya petroli  nchini.

Bei hiyo  itaanza kutumika kuanzia leo pamoja na kutambua bei kikomo ya   petroli nchi nzima.

Taarifa iliyotolewa na EWURA jana ilieleza kwamba bei ya mafuta ya aina zote yanayoingizwa kupitia Bandari ya Dar es Salaam  imepungua ikilinganishwa na toleo lililopita.

“Bei ya jumla na rejareja kwa mafuta ya aina zote (petroli, dizeli na mafuta ya taa) yaliyoingizwa nchini kupitia bandari ya Dar es Salaam imepungua ikilinganishwa na toleo lililopita la Januari 2, 2018.

“Kwa Februari 2019, bei za rejareja za petroli, dizeli na mafuta ya taa  imepungua kwa Sh 175/lita (asilimia 7.61),  Sh  144/lita (  asilimia 6.48) na Sh  156/lita (  asilimia 7.08), mtawalia.

“Vilevile  ikilinganishwa na toleo la mwezi uliopita, bei za jumla za petroli, dizeli na mafuta ya taa zimepungua kwa Sh 174.03/lita ( asilimia 8.02), Sh 143.65/lita (asilimia 6.84) na Sh  155.32/lita ( asilimia 7.47),  mtawalia.

“Kwa kiasi kikubwa, kupungua kwa bei za mafuta katika soko la ndani kunatokana na kuendelea kushuka kwa bei za mafuta hayo katika soko la dunia.

“Kwa mikoa ya kaskazini,  bei ya   petroli, dizeli na mafuta ya taa itaendelea kuwa  ile  ile ya   Januari 2019.

“Hii inatokana na ukweli kwamba pamoja na kuwa kuna shehena ya mafuta iliyopokelewa nchini  Januari 2019 kupitia bandari ya Tanga, mafuta hayo ni kidogo na hayatoshelezi mahitaji ya mafuta kwa mikoa yote ya kaskazini,” ilieleza taarifa hiyo

Hata hivyo taarifa hiyo ya EWURA ilieleza kwamba ghala ya kuhifadhia mafuta mkoani Tanga bado ina kiwango kikubwa cha mafuta yaliyopokelewa Desemba 2018 ambayo yatatosheleza mahitaji ya mafuta kwa mikoa ya kaskazini.

“Kwa hiyo, bei hizi za kuanzia Februari 6,  2019 zimezingatia gharama za mafuta yaliyoingizwa nchini Desemba 2018 kupitia Bandari ya Tanga,” ilieleza taarifa hiyo

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles