24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Waziri Mkuu aenda Kigoma kugawa miche ya michikichi

Na EDITHA KARLO  -KIGOMA 

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ameanza ziara ya siku moja mkoani Kigoma kwa ajili ya kugawa miche ya michikichi kwa makundi mbalimbali ya wakulima ikiwa ishara ya kuanza rasmi utekelezaji wa mkakati wa Serikali kuelekea kujitegemea kwa mafuta ya kula yatakayokuwa yakizalishwa kupitia zao la michikichi.

Mkuu wa Mkoa Kigoma, Emanuel Maganga akizungumza na waandishi wa habari Kigoma alisema mpango wa ugawaji wa miche hiyo utafanyika katika Gereza la Kwitanga Halmashauri ya wilaya Kigoma na kambi ya JKT Burombola kikosi cha 821 wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma.

Akizungumzia nafasi ya mkoa katika kusimamia utekelezaji wa mpango huo

Mkuu wa mkoa Kigoma, Emanuel Maganga alisema wataalam na watendaji wa mkoa huo wakishirikiana na taasisi mbalimbali wamejipanga kufanya uhamasishaji kwa wananchi, kutoa maelekezo na kufanya tathmini juu ya mpango huo na kwamba tayari wananchi wameonyesha ari kubwa ya

kushiriki kwenye utekelezaji huo.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Gerlad Kusaya alisema tayari miche milioni 1.8 ipo tayari kwa ajili ya kupandwa

mashambani ikiwa ni sehemu ya mpango wa uzalishaji na usambazaji kwa wakulima.

Alisema  miche milioni tano itapandwa kwenye mashamba ya

wakulima ili kufikia lengo la Tanzania kulima zao la  michikichi kwa

wingi kwa ajili ya kujitegemea katika uzalishaji wa mafuta ya mawese na kuondoa hali ya sasa ya kutumia shilingi bilioni 445 kuagiza mafuta hayo nje ya nchi.

Alisema katika mpango wa muda mrefu wa serikali kupitia wizara hiyo wanatarajia kuzalisha miche milioni 15 kwa mwaka na kuisambaza kwenye mashamba ya wakulima na kuwezesha Tanzania kufikia

lengo la kuzalisha tani 570,000  kwa mwaka ambazo zitatimiza ndoto ya nchi kuacha kuagiza mafuta hayo nje ya nchi.

Hii ni ziara ya nne ya Waziri Mkuu, Majaliwa kutembelea Mkoa Kigoma kwa ajili ya kukagua, kuhamasisha na kuona hatua zinazofikiwa katika utekelezaji wa mpango wa Serikali wa kuuchagua

Mkoa Kigoma kama mkoa kiongozi katika kilimo cha zao la michikichi na uzalishaji wa mafuta ya mawese.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles