27.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

WAZIRI AKERWANA RUSHWA VITUO VYA MIZANI

NA BENJAMIN MASESE- SHINYANGA

SERIKALI imewaonya wafanyakazi wa mizani nchini   kuacha vitendo vya vitendo vya rushwa kuleta tija na ufanisi wa kazi zao katika usimamiaji na ulinzi wa barabara.

Imesema ikiwa watumishi hao watafanya kazi  kwa weledi na  uadilifu Serikali  itaendelea kunufaika na miundombinu yake ya barabara na mizani ambayo imegharimu mabilioni ya fedha.

Onyo hilo lilitolewa    na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sektaya Ujenzi), Elias Kwandikwa.

Alikuwa   akikagua  mzani wa Tinde na Mwendakulima ambako  alikemea vitendo vya rushwa  vinavyofanywa kati ya  watumishi  na madereva wa malori na basi za abiria.

Waziri aliwataka watumishi hao kufuata sheria na taratibu za kiutumishi  na kuwaajibisha madereva wanaozidisha uzito na si kuomba rushwa.

Kwandikwa alisema kama wizara imepokea taarifa ya vitendo vinavyofanyika katika mizani mbalimbali na imeamua kupita kwa lengo la kuwaonya na kuwakumbusha kufuata sheria na taratbu za kiutumishi vinginevyo watawajibishwa.

Pia alisema wanatambua changamoto zinazowakabili na wanajipanga kushirikiana kwa pamoja kukaa na madereva  kuweza kutafuta suluhisho katika usimamiz wa mizani.

“Watumishi na madereva shirikianeni kutokomeza vitendo vya rushwa, kamwe msijihusishe kutoa wala kupokea rushwa  kupata huduma za haraka.

“Tukikubaini tutakuchukulia hatua kali za sheria, mambo yote yanayofanyika vituo kama hivi tumeyapata, hivyo badilikeni kabla ya hatua kuchukuliwa,”alisema.

Hata hivyo alitoa wito kwa madereva wa magari ya mizigo wanaotakiwa kuwa na stika maalumu za usafirishaji wa mizigo yao kufuata utaratibu wa kuchukua stika hizo mahali husika  kuepusha usumbufu na msongamano wa katika vituo vya mizani.

Akiwa katika eneo la sehemu ya maegesho  na kulaza magari mjini Kahama, Kwandikwa, alitoa wito kwa viongozi wa halmashauri hiyo kuchukua hatua kali kwa madereva wanaoegesha  nje ya eneo hilo  kudhibiti uchafuzi wa mazingira.

Alitoa ushauri kwa uongozi wa halmashauri hiyo kuona namna ya kujenga maegesho mengine kama hayo kupata chanzo cha mapato na kusaidia kuujenga mji kuwa na taswira nzuri.

Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Mkoa wa Shinyanga,   Mibala Ndilindi, alisema ni kweli vitendo vya  rushwa  vinafanyika katika vituo vya mizani.

Alisema  tayari hatua za sheria zimechukuliwa kwa watumishi watatu wa mizani ya Mwendakulima.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles