24.5 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

WAZIRI: AJIRA ZA AFYA ZINAKUJA

Na Walter Mguluchuma-Katavi

WIZARA ya Afya, Maendeleo ya   Jamii, Jinsia, Wazee na   Watoto, inatarajia kutoa   ajira kwa watumishi wa kada mbalimbali za afya.

Imesema watakaopewa  kipaumbele  ni wale wakataoomba  kufanya kazi mikoa ya pembezoni  ambayo ina upungufu mkubwa wa watumishi wa sekta hiyo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri  wa Afya, Maendeleo ya  Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy  Mwalimu,   wakati alipokuwa akihutubia wakazi wa Manispaa ya  Mpanda  mkoani    Katavi na kufungua upimaji na utoaji   tiba wa magonjwa yasiyoambukiza.

 

Alisema Serikali inatarajia kutangaza    ajira za watumishi 52,000 wa  kada  mbalimbali  hivi karibuni, hivyo kwa   nafasi za  ajira  zitakazotolewa zitagusa mikoa tisa.

Alisema watakaoomba kupangiwa   kufanya kazi Mkoa  wa Dares Salaam  hawatakuwa  na nafasi ya  kuchaguliwa  kwanza, kwani  mkoa  huo hauna tatizo kubwa.

Aliitaja  mikoa yenye uhaba wa wataalamu kuwa ni Katavi, Rukwa, Kigoma, Simiyu, Shinyanga, Tabora, Geita na Kagera.

Alisema tayari wizara yake imeandaa muswada  kwa ajili ya kuupeleka bungeni ili ujadiliwe na hatimaye uwe sheria itakayowezesha kila mtu  ajiunge na  Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Naye Mkuu wa Mkoa wa Katavi,  Meja Jenerali mstaafu Raphael  Muhuga, alisema Katavi  ina watumishi 692 kati ya 2,174 wanaohitajika.

Alisema kuna upungufu  wa  watumishi  1,186  sawa  na asilimia   69 ya mahitaji.

Ofisa Maendeleo ya Jamii wa  Mkoa wa Katavi, Anna Shumbi, alisema mkoa huo unaongoza kwa mimba za utotoni.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles