30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Watoto wamchanganya Rihanna

NEW YORK, MAREKANI 

STAA wa muziki wa pop nchini Marekani, Rihanna Fenty, ameonesha dalili ya kuhitaji mtoto baada ya rafiki yake Jennifer Rosales kujifungua mtoto wa kiume na kisha kumposti kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Mrembo huyo mwenye umri wa miaka 31, alianza kwa kumpongeza rafiki yake huyo kwa kujifungua salama na kisha kusema, anatamani siku moja na yeye aje kuitwa mama.

“Nina furaha kuona rafiki yangu amefanikiwa kupata mtoto, mimi nitakuwa shangazi yake, hivyo lazima ajue kuwa ninampenda sana.

“Ninakuwa na furaha nikiwa nawaona watoto wadogo, ninaamini na mimi ipo siku nitakuja kuitwa mama, sijui ni lini lakini muda utafika,” alisema msanii huyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles