30.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

WASAFIRI 1500 WAPIMWA EBOLA

NA VERONICA ROMWALD-DAR ES SALAAM


WASAFIRI 1,526 walioingia nchini wakitokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DCR) wamechunguzwa   afya zao dhidi ya  maambukizi ya   Ebola au la.

Hayo yalisemwa   Dar es Salaam jana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alipofungua semina ya kuwajengea  uwelewa juu ya ugonjwa huo.

Alisema wasafiri hao ni wale walioingia nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Uwanja wa Ndege Songwe, mipaka ya Rusumo, Mtukula na Kabanga.

Alisema taarifa zinaonyesha wasafiri wote waliochunguzwa hawakukutwa na maambukizi ya ugonjwa huo.

“Mlipuko wa sasa umetokwa eneo la Kivu Kaskazini kuna muingiliano mkubwa wa watu kutoka Kongo kwenda Uganda, Rwanda na Tanzania.

“WHO imeeleza tupo kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi” alisema.

Alisema takwimu zinaeleza tangu Agosti Mosi, mwaka huu ugonjwa huo uliporipotiwa kuwapo DRC    hadi sasa watu 116 wameripotiwa kuugua ugonjwa huo na 77 kati yao  wamefariki dunia.

Alisema lengo la serikali ni kuhakikisha ugonjwa huo hauingii  nchini lakini endapo utaripotiwa ni namna gani wamejiandaa usisambae.

“Nimeangalia madhara ya Ebola ilipotokea Afrika Magharibi (2013-16) biashara ilifungwa, mipaka na hata safari za ndege, jarida la The Times walitoa ripoti wakaeleza madhara ya Ebola yanagusa hadi uchumi wa nchi.

“Ugonjwa huu wa Ebola kwa kweli ni ugonjwa hatari, wanasema madhara ya uchumi juu ya Ebola yangeuwa watu wengi zaidi kuliko ugonjwa wenyewe.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles