23.3 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

WANYAMA WASABABISHA HASARA YA SH BILIONI 1.3

wanyama

Na  MALIMA  LUBASHA,

TEMBO, simba, chui, fisi na nungunungu  kutoka  Hifadhi  ya Taifa ya  Wanyama ya Serengeti  wamesababisha hasara  inayofikia Sh bilioni 1.3 kwa  kuvamia  makazi ya wananchi i  na kuharibu  ekari zipatazo 6,000 za mashamba, kujeruhi na kuua mifugo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira wilayani Serengeti,  Michael Kunani,    alisema  hiyo ni kwa mujibu wa  uchunguzi wa matukio ya wanyama hao  uliofanyika  kipindi cha kuanzia mwaka 2009 hadi 2016.

Alisema  uchunguizi huo umebaini kuwapo na  uharibifu wa mazao, mauaji ya mifugo ambako     wastani wa watu watatu huuawa kila mwaka katika vijiji vya Robanda, Singisi,Makundusi na Nyamatoke.

Matukio hayo i hutokea  wanyama hao wanapofika katika makazi ya wananchi na baadhi ya watu  wanapokwenda kufanya ujangili katika maeneo ya uhifadhi, alisema.

“Mwingiliano huo wa binadamu na wanyamapori umesababisha  kubadilika kwa tabia za wanyama hao kama tembo kwenda na kubomoa nyumba na kuangusha vihenge vinavyohifadhi nafaka hivyo kuongeza hasira kwa wananchi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles