27.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 18, 2024

Contact us: [email protected]

Wanawake Kagera hawanyonyeshi

breastfeedingHADIA KHAMIS NA YASSIN ISSAH, DAR ES SALAAM

MKOA wa Kagera unaongoza kwa kuwa na kiwango kikubwa cha kina mama wasionyonyesha watoto wa umri wa chini ya miezi sita, hali inayosababisha  udumavu wa akili kwa watoto hao, imeelezwa.

Hali hiyo pia inaufanya mkoa huo uongozwa kwa   vifo vingi vya watoto wenye udumavu na wa umri   chini ya miaka mitano.

kwa zaidi ya asilimia 40,kutokana na kukosa kunyonya ipasavyo imeelezwa.

Utafiti  uliofanywa na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania(TFNC) umeitaja mikoa mingine yenye kiwango kikubwa cha kina mama kutonyonyesha kuwa  ni Iringa, Njombe, Ruvuma, Rukwa, Kigoma, Katavi na Geita.

Takwimu hizo zilitolewa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Uzazi na Afya ya Mtoto katika Wizara  Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Dk. Georgina Msemo, Dar es Salaam jana.

Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari     katika uzinduzi wa Wiki ya Unyonyeshaji.

Dk. Msemo alisema   maadhimisho ya Siku ya Unyonyeshaji mwaka huu yatafanyika mkoani Kagera.

Alisema unyonyeshaji  maziwa ya mama pekee kwa mtoto chini ya miezi sita unasaidia kukuza akili ya mtoto na kupunguza magonjwa yasiyokuwa ya lazima.

Kulisha mtoto chini ya miezi sita vyakula vya nyongeza bado ni tatizo nchini.

Alisema  takwimu zinaonyesha   asilimia tano ya watoto   chini ya miezi sita wanapewa chakula au vinywaji kwa kutumia chupa.

Dk. Msemo alisema utafiti unaonyesha  asilimia 32 na 24 ya watoto wanaozaliwa vijijini na mijini hupewa kinywaji au chakula kingine hata kabla ya kuanzishiwa maziwa ya mama.

“Utafiti huo unaonyesha kuwa ni asilimia 50 tu ya watoto wa umri wa mwezi 0 mpaka sita hunyonyeshwa maziwa ya mama pekee.

“Wakati huo huo takwimu zinaonyesha  asilimia 81 ya watoto wa   miezi miwili hunyonyeshwa maziwa ya mama pekee,” alisema.

Alisema idadi ya watoto wanaonyonyeshwa maziwa ya mama pekee huendelea kupungua kadri umri unavyoongezeka.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa  TFNC, Dk.Sabas Kimboka, alisema Tanzania imefanya juhudi kubwa   kuboresha   ulishaji wa watoto wachanga na wadogo, lakini hali   bado hairidhishi.

Alisema asilimia 97 ya wanawake   nchini hunyonyesha watoto wao, lakini unyonyeshaji huo haufuatwi ipasavyo.

“Utafiti wa hali ya demografia na afya nchini mwaka 2010, unaonyesha   unyonyeshaji wa maziwa ya mama ndani ya saa moja ya kwanza baada ya kujifungua ni asilimia 49 ikilinganisha na asilimia 59 ya  mwaka 2005.

“Hali hii huchangiwa kwa kiasi kikubwa na idadi ndogo ya wanawake wanaojifungulia katika vituo vya afya ambao ni asilimia 50,”alisema Dk.Kimboka.

Alisema utafiti mbalimbali unaonyesha  asilimia 58 ya wanawake waliojifungua kwa usaidizi wa wauguzi wenye elimu na ujuzi, wana uwezekano mkubwa wa kuwanyonyesha watoto wao ndani ya saa moja, kuliko waliozalishwa na wakunga wa jadi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles