23.8 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Waliokunywa pombe ya sumy wafikia 325

Togwa
Togwa

Na Amon Mtega, Songea

IDADI ya wakazi  wa Kijiji cha Litapwasi Wilaya ya Songea  mkoani Ruvuma waliolazwa hospitalini wakidaiwa kunywa togwa yenye sumu imeongezeka kutoka 246   kufikia 325.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Mihayo Msikhela, alisema jana wanakijiji hao wamelazwa katika   Hospitali ya Peramiho na zahanati ya Lyangweni iliyopo kijijini hapo.

Alisema kutokana na tukio hilo jeshi la polisi linawashikilia watuhumiwa kadhaa  huku baadhi ya wagonjwa wakiruhusiwa kurudi makwao baada ya afya zao kuimarika.

Kamanda alisema tukio hilo   lilitokea Septemba 28 mchana katika sherehe ya Kipaimara ya mtoto Dickson Nungu (14) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Litapwasi.

Alisema polisi wanaendelea kufuatilia tukio hilo na  wamekwisha kuchukua sampuli ya mabaki ya vyakula na togwa ambavyo vimepeleka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali Dar es Salaam kwa uchunguzi.

Kamanda Msikhela alisema jeshi lake linawashikilia watu watano kwa   mahojiano   akiwamo mwandaaji wa sherehe hiyo.

Aliwataja watu wanaoshikiliwa na polisi kuwa ni   Enesi Nungu (47) mkazi wa kijiji hicho ambaye ndiye mwandaaji wa sherehe hiyo.

Wengine ni  Benidict  Nungu (76), Esebius Komba (36), Sadiki Masoud (65) na  John Kaulangudidi Mapunda, wote wakazi wa kijiji hicho.

Baadhi ya majeruhi waliolazwa katika Hospital ya Misheni ya Peramiho walisema walipatwa na masahibu hayo baada ya kunywa togwa iliyoandaliwa katika sherehe ya kipaimara ya mtoto wa mwanakijiji mwenzao.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles