25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Wajasiriamali wakopeshwa mil 52/-

Kaimu Mkurugenzi wa manispaa hiyo, Raphael Kimary
Raphael Kimary

NA AMON MTEGA, SONGEA

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, imetoa mkopo wa Sh milioni 52 kwa vikundi 107 vya wajasiriamali ili kuendeleza miradi yao.

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo ya vikundi hivyo juzi, Kaimu Mkurugenzi wa manispaa hiyo, Raphael Kimary, aliwaasa wajasiriamali hao kuwa na nidhamu ya matumizi ya mikopo ili mwisho wa siku wahakikishe wanairejesha kwa wakati.

Alisema mkopo huo umetolewa na manispaa kwa lengo la kusaidia vikundi vya wajasiriamali  katika shughuli za uwekezaji  na kuhakikisha wanainua kipato chao cha kila siku.

Kwa upande wake Ofisa Maendeleo ya Jamii wa manispaa hiyo, Naftali Saiyoloi, alisema mkopo huo una lengo la kuinua hali ya uchumi katika makundi hayo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles