33.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Wagombea wenza Marekani wajiandaa kwa mdahalo wao

usa-jp

Madison, Wisconsin

MGOMBEA urais wa Marekani kwa tiketi ya Republican, Donald Trump na mgombea wa Democratic, Hillary Clinton wakijigamba kufanya vizuri katika mdahalo wao, wagombea wenza nao wanajiandaa kushindana.

Tofauti na wagombea wenyewe, mada za wagombea wenza katika mjadala hautatangazwa na tume ya mijadala ya marais kwa hiyo Mike Pence wa Republican na Tim Kaine wa Democratic hawana haja ya kujiandaa.

Pence aliwaambia wafuasi wake kwamba alikuwa amejiandaa vyema kwa mdahalo.

Kaine alitumia muda wake akiwa Raleigh, Carolina Kaskazini akijiandaa na mdahalo huo.

Wiki ijayo Trump na Clinton wanatarajiwa kushiriki katika mdahalo wa pili kati ya mitatu inayotarajiwa kufanyika kabla ya Wamarekani hawajafanya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Novemba 8, mwaka huu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles