24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

WAFANYABIASHARA MBARONI WAKITUHUMIWA KUBAKA WANAFUNZI

teen-in-handcuffs-shutterstock-800x430

Na JANETH MUSHI-ARUSHA

JESHI la Polisi Mkoa wa Arusha linawashikilia wafanyabiashara wawili wakazi wa Kata ya Daraja Mbili jijini Arusha kwa tuhuma za kuwabaka wanafunzi wanne (majina yanahifadhiwa) wa shule tatu tofauti za msingi,wanaokadiriwa kuwa na umri wa miaka 11 hadi 12.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo, tukio hilo lilitokea Desemba 30, mwaka jana katika Kata ya Daraja Mbili.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Aloyce January (23) na Daniel William (26) ambao wanadaiwa kuwabaka wanafunzi hao wanaosoma Shule ya Msingi Themi, Daraja Mbili na Uhuru na kuwasababishia maumivu makali katika miili yao.

Alisema kuwa uchunguzi wa awali ulibaini kuwa watoto hao waliitwa ndani ya nyumba wanayoishi watuhumiwa na kuwaambia kuwa wanataka kuwatuma, lakini baada ya kuingia waliwatisha na kuwaambia wasipige kelele na endapo wangefanya hivyo wangewachoma visu.

“Baada ya watoto kutishwa iliwalazimu kunyamaza kimya na kufanyiwa kitendo hicho cha kuingiliwa kimwili na kuwasababishia maumivu makali,” alisema Kamanda Mkumbo.

Alisema baada ya tukio hilo, taarifa zilifika Kituo Kikuu cha Polisi Arusha, ambapo Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na raia wema lilifanya uchunguzi na kuwakamata watuhumiwa hao.

Kamanda Mkumbo alisema kuwa wanafunzi hao walichukuliwa kwa mahojiano na watuhumiwa wapo chini ya ulinzi na kwamba upelelezi utakapokamilika watafikishwa mahakamani.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles