25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

WABUNGE CHADEMA ‘WAMKIMBIA’ CHIZA AKIAPA BUNGENI

|Mwandishi Wetu, Dodoma



Wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wametoka ndani ya Ukumbi wa Bunge wakati Mbunge wa Buyungu, Christopher Chiza (CCM), akiapa.

Tukio hilo lilitokea mapema asubuhi leo wakati baadhi ya wabunge hao wakiwa  ukumbini tayari kwa kuanza kwa kikao cha bunge lakini walitoka kabla Spika Job Ndugai, hajaingia na kisha kuingia baada ya Ciza kula kiapo cha uaminifu.

Hali hiyo ilisababisha viti vya upande wanaokaa wabunge hao kuonekana vitupu huku wakonekana baadhi ya wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF).

Chiza ameapa leo baada ya kushinda ubunge wa Jimbo la Buyungu baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Kasuku Bilago kufariki dunia.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles