27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Vifaa vya Sh bilioni 1.2 kuimarisha ulinzi Hifadhi ya Ruaha

Francis Godwin, Iringa

VIFAA  mbali  mbali vyenye thamani ya  Sh bilioni 1.2  vimetolewa  katika  Hifadhi ya Taifa ya  Ruaha Iringa  kwa ajili ya   kuimarisha  ulinzi  dhidi ya majangili katika  hifadhi  hiyo.

Mratibu wa mradi wa mradi wa Kuendeleza Utalii Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (REGROW), Saanya Saenea, alisema  juzi wakati wa  hafla ya  kuzindua  vifaa  hivyo iliyofanyika katika  ofisi   za hifadhi ya  Ruaha  mkoani hapa alisema ifaa  hivyo vimetolewa   kwa  ajili ya  kuongeza  nguvu ya ulinzi kwenye  hifadhi  hiyo.

Alisema  mradi  huo  wa Regrow  umeanza kazi kwa  kasi na  kupitia vitendea  kazi mbali mbali  vya ulinzi ambavyo  vimetolewa  wanauhakika  ulinzi  utaimarishwa zaidi  kwenye  hifadhi  hiyo .

Pia  alisema  kupitia mradi  huo  watahakikisha   wanaweka  mikakati ya  kunusuru kukauka kwa mto Ruaha mkuu  ambao  ni  mto tegemeo kubwa kwa  wanyama  hivyo  wananchi  wanaozunguka  hifadhi  hiyo  watajengewa mabwawa na elimu ya umwagiliaji wenye tija itatolewa.

Katibu Mkuu  wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Profesa Adolf Mkenda  alisema  wizara yake imejiwekea kipaumbele cha  kuboresha miundo mbinu ya hifadhi za ukanda wa kusini na zile mpya zilizoanzishwa hivi karibuni na kuzitangaza ulimwenguni kote.

Alisema  uimarishaji  wa miundo  mbinu katika hifadhi utaongeza  kasi  kubwa ya  watalii nchini  na kuwa  kazi kubwa  ni  kuona  hifadhi  hizo  zinaendelea  kutangazwa  zaidi ndani na nje na utangazaji  wake  uwe ni ule wenye  tija .

Kamishna Mwandamizi wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi  za  Taifa  (TANAPA ) Kanda ya  Kusini, Dk.Christopher Timbuka , alisema  ujio wa mradi wa REGROW  umetokana na changamoto ambazo hifadhi  za kusini  zilikuwa  zikikabiliwa  nazo .

Alisema miundombinu  kuwa mibovu na  watalii kushindwa kufika katika  hifadhi   hivyo mradi huo  utawezesha kufungua  utalii   nyanda  za  kusini .

 Alisema  ujio wa mradi huo  ambao unaanza kazi  utasaidia  kuongeza idadi ya watalii na kuongeza idadi ya  vitanda  kutoka  vitanda  400  vilivyopo na kuongezeka zaidi ili  watalii  kuweza kupata maeneo ya  kufikia .

 Alisema  kupitia  mradi huo  ulinzi  ulinzi  didhi ya ujangili  kwenye hifadhi  utapungua zaidi  kutokana na mradi  huo  kuwezesha  vitendea kazi vya  kisasa kwa ajili ya kuimarisha  ulinzi .

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles