25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Vazi la Kim Kardashian, Rihanna lashangaza wengi

Kim Kardashian na kanyeruhanaBADI MCHOMOLO NA MITANDAO
MAVAZI ya mwanamuziki Rihanna na mwanamitindo, Kim Kardashian yamekuwa kivutio na kituko kwa mashabiki wao walipokuwa katika onyesho la Met Gala, huko nchini Marekani.
Kim alikuwa karibu muda wote na mume wake mwanamuziki, Kanye West, huku Rihanna akiwa wa mwisho kuingia katika onyesho hilo akionekana mpweke aliyefunikwa vema na gauni lake lililoonekana kama limemkumbatia.
Wawili hao walionekana katika onyesho la Met Gala, lililohudhuriwa na wasanii wa fani mbalimbali, lakini hata hivyo hawakujali namna watu walivyokuwa wakiwazungumzia.
“Nimeamua kuacha simu yangu nyumbani kwa kuwa nilijua kwamba mashabiki watakuwa na maswali mengi juu ya vazi langu,’’ alisema Kim na kuongeza:
“Nikiwa na shida ya kutumia simu nitatumia ya mume wangu, ninaamini kama ningekuja na simu yangu muda mwingi ningekuwa natumia kutokana na ujumbe kutoka kwa mashabiki.”

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles