27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

UN YAONYA MATAIFA YENYE NGUVU MZOZO WA SYRIA

UN, NEW YORK


UMOJA wa Mataifa (UN) umezionya nchi zenye nguvu zaidi duniani kutochochea mzozo wa madai ya matumizi ya silaha za sumu dhidi ya raia nchini Syria.

Kauli hiyo imekuja baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema makombora yanakuja nchini Syria.

Kufuatia hali ya taharuki kuhusiana na mzozo huo wa Syria, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa jana lilikutana kwa kikao cha dharura kujadili hali hiyo ya Syria.

Aidha Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May ameitisha kikao cha dharura cha baraza lake la mawaziri kujadili uwezekano wa nchi hiyo kuhusika katika operesheni ya kijeshi dhidi ya utawala wa Syria.

Ni baada ya kuutuhumu utawala huo na washirika wake Urusi kutumia silaha za sumu dhidi ya raia katika mji wa Douma.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres, Baraza la Usalama la umoja huo mpaka sasa limeshindwa kufikia suluhisho la kidiplomasia kuhusu Syria.

Kwa sababu hiyo ametoa wito wa nchi wanachama wa kudumu wa baraza hilo Marekani, Urusi, China, Ufaransa na Uingereza kutakafakari kwa undani na kuchukua hatua madhubuti ambazo haitauchochea zaidi mzozo wa Syria.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles