31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Ummy Mwalimu: Hatuna mgonjwa wa corona

AVELINE   KITOMARY

Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inamwewatoa hofu  wananchi kutokana na taarifa zilizoenea ya kupatikana kwa wagonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na Virusi hatari vya Corona  Mkoani Kilimanjaro.

Taarifa iliyotolewa na Waziri wa Afya  Ummy Mwalimu zilisema kuwa mnamo Machi 13  mwaka huu  katika kiwanja cha ndege cha Kimataifa  cha Kilimanjaro (KIA) wasafiri sita walipokelewa  wakitokea nchini Kenya.

“Ninapenda kutumia fursa hii kuwatoa hofu wananchi  hadi sasa nchi yetu  hakuna  mgonjwa wa maambukizi ya virusi vya Corona (COVID 19),  Wasafiri hao  Walikuja kwa  ndege ya Precious Airv PW722, wageni hao wanne walikuwa raia wa Denmark na wawili ni raia wa Norway wanawake walikuwa watano na wanaume mmoja.

“Hata hivyo baada ya ukaguzi  wa joto la mwili (screening) uliofanywa na maofisa wetu  wa afya katika kiwanja hicho  waligundua mmoja wao kuwa na homa ya nyuzi joto 38 pamoja na kikohozi na kuchoka,” ilisema Taarifa hiyo.

Taarifa hiyo pia ilisema  kuwa wasafiri hao walitengwa na kupelekwa kwenye eneo maalum  la kuwatenga washukiwa  wa magonjwa ya mlipuko  katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro(Mawenzi).

“katika kuwahoji  zaidi wasafiri hawa , maafisa wetu walibaini kuwa msafiri mmoja alikuwa na historia ya kukohoa  lakini hakuwa na homa  hata hivyo wasafiri wote sita walichukuliwa sampuli kwa kuwa walikuwa wakisafiri wote pamoja  ambapo sampuli hizo zilipelekwa  kwenye maabara ya Taifa ya Afya  ya Jamii  iliyopo Dar es Salaam kwaajili ya uchunguzi .

“Uchunguzi wa maabara ulibaini kuwa wasafiri wote hawakuwa na maabukizi  ya virusi vya corona aidha msafiri aliyekutwa na joto kali  alibainika kuwa na mafua ya kawaida  hadi sasa hali za wasafiri wote wako salama  na wameruhusiwa kufanya shughuli zao.

Hata hivyo taarifa hiyo ilitoa rai kwa wananchi kutokusambaza taarifa ambazo hazijathibitiswa na serikali .

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles