25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

ULANGA, KILOMBERO WAPITISHA MPANGO WA ARDHI

William Lukuvi
William Lukuvi

Na Ramadhan Libenanga-Kilombero

VIJIJI sita vilivyopo katika wilaya za Kilombero na Ulanga mkoani Morogoro vimepanga na kupitisha mpango wa matumizi bora ya ardhi ikiwa ni utekelezaji wa mpango wa kuwezesha umilikishaji ardhi katika vijiji vyote vya wilaya hizo.

Maamuzi hayo yamefanyika katika mikutano mikuu ya hadhara ya vijiji hivyo ambapo licha ya kupitisha mpango huo pia wamepitisha sheria ndogo ambazo zitawabana wale wote watakaokiuka sheria walizojiwekea ili kupunguza migogoro ya ardhi.

Akizungumza katika mikutano hiyo, Ofisa Ardhi wa Wilaya ya Kilombero,  Siyabumi Mwaipopo alisema  katika kufanikisha kupitisha mpango huo walishirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na wataalamu kutoka mpango wa kuwezesha umilikishaji ardhi (LTSP), sasa hatua hiyo itasaidia kulinda haki za wananchi katika umiliki wa ardhi.

Alisema LTSP walianza kuhamasisha wananchi hasa makundi maalumu hasa ya wanawake, vijana, wafugaji, watu wenye umelavu jambo ambalo litasaidia utekelezaji wa mpango huo wa matumizi bora ya ardhi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles