24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Tsvangirai: Fedha mpya si suluhu kiuchumi

Morgan-Tsvangirai1HARARE, ZIMBABWE

KIONGOZI wa chama cha upinzani nchini Zimbabwe, Movement for Democratic Change (MDC) kinachoongozwa na Morgan Tsvangirai, amesema kuanzishwa kwa fedha ya dhamana si suluhisho la tatizo la uchumi.

Katika taarifa iliyotolewa na msemaji wake, Luke Tamborinyoka, alisema tatizo la uchumi ni matokeo ya hali ya sintofahamu iliyoanzia wakati wa uchaguzi uliovurugwa mwaka 2013.

“Bahati mbaya, kitendo cha chama tawala cha Zanu PF kuchapisha noti mpya hakiwezi kuwa dawa kwa tatizo la kisiasa linalohitaji suluhu ya kisiasa.

“Hizo noti za dhamana ni ushahidi wa ukatili wa Serikali inayong’ang’ania kuongoza nchi,” alisema Tamborinyoka.

Wiki iliyopita, Gavana wa Benki Kuu ya Zimbabwe (RBZ), John Mangudya, alitangaza kuwa Zimbabwe itaanzisha noti mpya za fedha ya dhamana ili kuziba pengo la fedha linaloikabili.

Fedha hizo zitadhaminiwa kwa dola milioni 200 na Benki ya Afrexibank iliyopo Misri.

Lakini pia Tsvangirai alisema Serikali imetumia mlango wa nyuma kuirudisha dola ya Zimbabwe na kwamba itairudisha nchi katika zama za mfumuko mkubwa wa bei ulioshuhudiwa miaka minane iliyopita.

Alisema chama chake kitakutana haraka kuzungumzia suala hilo na kinapanga kuanzisha maandamano makubwa kupinga mpango huo.

Hatua hiyo ambayo RZB imekiri kuwa fedha hizo hazitaweza kununua chochote nje ya nchi, imewatia hofu wananchi ambao wameanza kuondoa fedha zao benki.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles