23.8 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

TIMU ZAONYWA MECHI ZA KIMATAIFA ZA KIRAFIKI

Na THERESIA GASPER,DAR ES SALAAM



MKURUGENZI wa Mashindano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Salum Madadi, amezitaka timu za soka zinazoalika timu za nje kwa michezo ya kirafiki kufuata taratibu.

TFF imetoa agizo hilo kutokana na hivi karibuni Simba kuialika AFC Leopards ya Kenya na Biashara United kuwaalika Sony Sugar na kucheza nao mechi za kirafiki nchini.

Akizungumza na  waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Madadi alisema kutokana na uwepo wa mialiko isiyofuata utaratibu, wameamua kuziandikia timu hizo na vyama vyote vya soka nchini kuwataka kufuata kanuni.

“Tumeandika barua kwa wanachama wetu na mashirikisho ya soka kutokana na mialiko ya hivi karibuni ya timu mbili za Kenya, Leopads na Sony Sugar, kuna baadhi ya mechi tumezuia  zisichezwe kutokana na kutokukamilika kwa  taratibu za mwaliko wa timu hizo,” alisema Madadi.

Alisema hairuhusiwi  timu ya soka kutoka nje ya nchi kucheza mechi ya kirafiki au kushiriki mashindano mbalimbali bila kupata kibali kutoka katika chama au shirikisho la  soka la nchi inayotoka.

“Tunafanya hivyo kwa sababu  tuliwahi kupata adhabu ya kulipa faini FIFA kutokana na timu ya Twiga Stars  kuongeza mchezo wa pili Cameroon bila kufuata taratibu baada ya kualikwa,” alisema Madadi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles