23.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

TFDA YAFUTA USAJILI   DAWA ZENYE MADHARA

Na Prisca Libaga -Arusha.

MAMLAKA ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA)  imezifutia usajili dawa mbalimbali za kutibu magonjwa ya binadamu.

Vilevile imeziondoa  kwenye soko   na kusimamisha  matumizi yake  kutokana na kuwa na madhara makubwa kwa wagonjwa.

Hayo yalielezwa   Arusha jana na Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo, alipofungua mafunzo ya wakufunzi  wa kufuatilia kufundisha na kuhamasisha  masuala ya udhibiti  wa madhara yanayotokana na matumizi ya dawa zisizosalama kwa watendaji wa afya kutoka wilaya zote za mkoa wa Arusha.

Alisema katika kudhibiti matumizi ya dawa zisizofaa, TFDA imeondoa  dawa ya sindano   ya Chloramphenical  kwenye soko  baada ya Shirika la Afya Duniani (WHO)  kubaini   ina  madhara  kwa watumiaji.

Mamlaka  pia   imefuta usajili wa dawa  nyingine ambazo ni Ketoconazole (vidonge) Phenylpropanalamine, Dextropropoxyphene, Nimesulide, stavudine 40, Gatifloxacin, Rofecoxib  na Celecoxib baada ya kuthibitika zina madhara kwa watumiaji.

Alisema matumizi ya dawa kama   Kanamycin, Amikacin na Levofloxacin  yamebadilishwa    ziweze kutumika    kutibu ugonjwa  wa kifua kikuu pekee.

Mkurugenzi huyo wa TFDA alisema mafunzo hayo yanashirikisha wakufunzi 60 nchini kote na yanafanyika katika mikoa mbalimbali  yakiwashirikisha madaktari, wauguzi na wafamasia  walioko kwenye  hospitali, vituo vya afya na zahanati.

Alisema lengo la mafunzo hayo ni kuongeza idadi ya wakufunzi wa masuala ya usalama wa dawa  kutoka 73  hadi 133.

Alisema   katika kipindi cha miaka mitatu 2014/ 15 hadi 2017/18, TFDA imehamasisha watendaji wa afya wapatao 2000 nchini kote na sasa uhamasishaji unaendelea  katika Mkoa wa Katavi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles