25 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

TBL Group kufadhili elimu ya ufundi kwa vijana

Meneja wa Mafunzo wa TBL Group, Gasper Tesha
Meneja wa Mafunzo wa TBL Group, Gasper Tesha

Na Veronica Romwald, Dar es Salaam

KAMPUNI ya TBL Group imeahidi kuendelea kuwaunga mkono vijana wa Tanzania kwa kuwawezesha kupata elimu ya ufundi stadi katika vyuo vya Veta kupitia mpango maalumu wa kupata elimu zaidi ya vitendo kuliko nadharia unaojulikana kitaalamu kama ‘Dual Apprenticeship programme’.

Mpango huo  unaoendeshwa na Serikali kupitia taasisi zake za mafunzo ya ufundi kwa kushirikiana na Chama cha Wenye Ujuzi cha Hamburg, Ujerumani.

Mpango huo umelenga kuwapatia vijana elimu na mafunzo kwa vitendo ambapo watasoma huku wakiwa wanapatiwa mafunzo ya vitendo kwenye viwanda na taasisi mbalimbali.

Akizungumzia mpango huo ulioanzishwa miaka mitatu iliyopita, Meneja wa Mafunzo wa TBL Group, Gasper Tesha, alisema umeonyesha maendeleo mazuri na makubwa ikiwa ni pamoja na kuwanufaisha vijana hao katika utendaji kazi sehemu mbalimbali kutokana na ujuzi waliopatiwa.

Tesha alisema vijana wanne waliofadhiliwa na kampuni hiyo na kupatiwa mafunzo katika fani ya umeme wa viwandani, wameweza kupata maarifa makubwa ya kazi kwa vitendo kwenye kiwanda cha TBL cha Ilala na baada ya kuhitimu masomo  wameajiriwa.

“Hivi sasa kumekuwepo dhana ya  waajiri wengi kuangalia vyeti badala ya ujuzi, hali ambayo kwa fani ya ufundi kunahitajika mafunzo ya vitendo kwa kiasi kikubwa ili wahitimu wa mafunzo hayo waweze kukubalika kwenye soko la ajira.  Changamoto hii ni kubwa hapa nchini kwa kuwa wahitimu wengi wa fani za ufundi wanakuwa na mafunzo ya nadharia tu  na wanapopata ajira wanashindwa  kumudu kazi walizosomea na kukidhi matakwa ya waajiri wao,” alisema Tesha.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles