27.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 18, 2024

Contact us: [email protected]

TAEC yasaini mkataba ujenzi maabara ya kisasa

Mwandishi Wetu, Arusha

Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC), iko mbioni kuanza ujenzi wa awamu ya pili ya maabara kisasa itakayojengwa na Kampuni ya Ujenzi ya M/S Li Jun Development Construction Ltd.

Tayari tume hiyo imesaini mkataba wa Sh bilioni 10.474 kwa ujenzi wa maabara hiyo itakayojengwa kwenye Makao Makuu ya TAEC, yaliyopo Njiro jijini Arusha.

Mkurugenzi Mkuu wa TAEC, Profesa Lazaro Busagala ameitaka kampuni hiyo kuhakikisha inajenga maabara hiyo kwa kiwango cha hali ya juu kulingana na makubaliano ya mkataba husika.

“Maabara hii ni mwendelezo wa maabara ya awamu ya kwanza iliyozinduliwa Aprili  mwaka huu na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na pia ujenzi huu ni juhudi nyingine za serikali katika kuendelea kuleta maendeleo nchini,” amesema Profesa Busagala.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles