24.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

STARS YAIVAMIA SUDAN

MOHAMED KASSARA-DAR ES SALAAM

KATIKA kuthibitisha kuwa imepania kupindua meza, kikosi cha timu ya Taifa Tanzania ‘ Taifa Stars’,  tayari kimetua Sudan,  kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa kusaka tiketi ya kufuzu Fainali za Mataifa ya

Afrika kwa Wachezaji Wanaocheza Ligi za Ndani(Chan), utakaopigwa Ijumaa hii jijini Khartoum.

Timu hizo zilipoumana katika mchezo wa kwanza uliochezwa Septemba 22, Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Sudan iliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Stars.

Ili kuishinda Sudan na kutinga hatua ya makundi, Stars itatakiwa kupata ushindi wa kuanzia mabao 2-0, zitakaporudiana  kesho kutwa.

Kikosi cha Stars kiliondoka Kigali juzi usiku kwenda Khartoum, baada ya mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Rwanda  uliochezwa Uwanja wa Amahoro na kumalizika kwa suluhu.


Mchezo huo huo wa kujipima ubavu ulikuwa kukidhi matakwa ya Kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).

Mchezo wa marudiano kati  ya Stars na Sudan  utakaopigwa Uwanja wa Omdurman, wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 65,000.

Sababu ya kikosi cha Stars kuunganisha moja kwa moja Sudan, zinalengwa na kuwapa muda wa kuzoea hali ya hewa wachezaji wa kikosi hicho.
Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo wao na  Rwanda juzi, Kaimu Kocha Mkuu wa Stars, Etienne Ndayiragije alisema aliridhishwa na suluhu waliyoipata na kudai kuwa, mchezo dhidi ya Rwanda ulikuwa  kipimo sahihi kwao .

“Nashukuru kwa mchezo kumalizika salama, nimeridhishwa na kiwango kilichoonyeshwa na wachezaji wangu, nakiri  kwamba tulipata mtihani sahihi kulingana na kazi  iliyo mbele yetu.

“Mchezo huu utatusadia sana katika maandalizi yetu kuelekea mechi ya marudiano na Sudan, kuna vitu vichache vya kufanyia kazi na bado tuna muda wa kurekebisha, lakini vijana walicheza kwa kufuata maelekezo yangu, nimefurahishwa na hali hiyo,” alisema kocha huyo raia wa Burundi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles