30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Simba bado yajivuta kumtangaza kocha

simba scNA ADAM MKWEPU, DAR ES SALAAM

WAKATI mashabiki wa timu ya Simba wakiwa na shauku kubwa kutaka kujua ujio wa kocha mkuu wa timu hiyo, uongozi wa klabu hiyo umewatuliza presha kwa kuahidi  kumtangaza  rasmi kocha mpya ndani ya wiki mbili kabla ya kuanza michezo ya kirafiki  ya kujiandaa na msimu mpya wa 2016/17.

Simba bado wanaumiza  kichwa kufanya uamuzi wa kupata saini  ya kocha mmoja kati ya makocha  wawili  wa kimataifa  ambaye  ataweza  kuiletea mafanikio timu hiyo msimu ujao, akiwamo aliyekuwa kocha  wa timu ya taifa ya Kenya  Mscotlandm Bobby Williamson na mwingine ambaye jina lake halikutajwa.

Kocha huyo ana kila dalili ya kutua Msimbazi kipindi hiki cha usajili kwa ajili ya msimu ujao, kutokana na hali iliyopo ndani ya benchi la ufundi la Kenya ambapo kwa sasa Shirikisho la soka la nchi hiyo ‘KFF’, limempa  madaraka ya kuiongoza timu hiyo ya taifa kocha mzawa, Stanley Okumbi, akisaidiwa na Mussa Otieno.

Taarifa toka ndani ya klabu ya Simba, zinadai kwamba baada ya mipango yake ya kupata saini ya kocha wa Taifa wa Zimbabwe, Kalisto Pasuwa, kuvurugika  ipo kwenye mazungumzo  ya mwisho na makocha hao akiwamo Bobby.

“Tulikaribia kuipata saini ya Pasuwa  ambaye  alikuwa chaguo letu la kwanza, lakini kutokana na mkataba wake  kuwa  wa muda mrefu pia timu yake kufuzu katika fainali za mataifa ya Afrika, Afcon hivyo ikawa kikwazo  kwetu, hata hivyo hatujakata tamaa na tunaahidi kupata kocha bora, tunawataka mashabiki watulie, safari hii hatutafanya makosa  kama yaliyopita, tutafanya uamuzi  sahihi kwa ajili ya mafanikio ya Simba.

“Ndani ya wiki mbili kila kitu kitakuwa wazi pamoja na majina ya wachezaji wapya ambao tayari tumeshawasajili kwa ajili ya msimu ujao.

“Tutasajili wachezaji kulingana na uhitaji wa klabu kwa kuangalia eneo lenye mapungufu ndani ya kikosi cha Simba,” kilisema chanzo hicho.

Chanzo hicho kilisema kwamba, hadi sasa klabu hiyo imewasajili wachezaji watano ambao ni beki wa kati, Emmanuel Semwanza, Hamad Juma, Ramadhani ‘Chiza’ Kichuya, Muzamil Yassin na Jamal Mnyate kutoka  Mwadui FC inayonolewa na Jamhuri Kihwelu ‘Julio’.

“Tunafanya mambo yetu kwa utulivu wa hali ya juu, ndio maana tunasajili wachezaji wapya kwa uangalifu mkubwa ili kuepusha hujuma msimu ujao,” kilisema chanzo hicho

- Advertisement -
Previous article
Next article

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles