24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Shigella awataka wafanyabiashara kuchangia mapambano dhidi ya corona

Mwandishi Wetu, Tanga

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella amepokea vifaa vya kujikinga na maambukizi ya virusi vya ugonjwa wa corona na kuwataka wafanyabiashara wengine kuguswa na kuchangia ili kuhakikisha wanadhibiti maambukizi mkoani humo.


Shigela amesema hayo leo wakati akipokea msaada wa matanki matano yenye ujazo wa lita 500 kila moja kutoka kampuni ya vifaa vya ujenzi ya Hussein plastic Industry ya Jijini Tanga.


Amesema bado kuna uhitaji mkubwa wa vifaa hivyo katika maeneo mengi mkoani humo.


“Licha ya kwamba bado kama mkoa hakuna mgonjwa hata mmoja lakini tumeona iko haja ya kuendelea kutii maagizo ya wataalamu wa afya juu ya kuchukua tahadhari ya ugonjwa huo,” amesema Shigella.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Yusuf Tayabali amesema wameamua kutoa msaada huo ili kuunga mkono juhudi za serikali katika mapambano ya ugonjwa huo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles