30.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

SERIKALI YAWATAKA VIJANA KWENDA VETA KUPATA UJUZI

Na  SAMWEL MWANGA – BARIADI


WAZAZI na walezi wametakiwa kuwahamasisha vijana wao kujiunga na vyuo vya  Mafunzo ya Elimu ya Ufundi Stadi (VETA)  kuchangamkia fursa za ujuzi katika fani mbalimbali.

Wito huo ulitolewa na Meneja Uhusiano  wa  VETA, Sitta Peter alipozungumza na wadau mbalimbali wa
maendeleo b mjini Bariadi.

Alisema  vijana wengi nchini  wamekuwa wakibaki nyuma na kushindwa kwenda vyuo vya ufundi  kupata ujuzi ikizingatiwa shughuli nyingi za maendeleo kupitia miradi mbalimbali inahitaji watu wenye ujuzi.

Peter alisema  fursa   nyingi ambazo zinazotokana na ujuzi zimekuwa zikichangamkiwa na wageni kutoka nje ya nchi huku wenyeji wakibaki nyuma  na  kuendelea kulalamikia serikali juu ya ukosefu wa ajira.

‘’Asilimia 90 ya wanafunzi walioko katika  vyuo vyetu si wazawa wa mikoa ya  Shinyanga, Mara na Mwanza ispokuwa waliopo wanatoka mikoa ambayo haina vyuo, tunaomba  jamii iwe na mwamko wa kuwapeleka  watoto  veta.

“Vijana walioko katika vyuo vyetu wahakikishe mafunzo wanayoyapata yanageuka kuwa mali kwa kuitumia kama fursa ya kuweza kujiajiri na kupambana na umasikini katika ngazi ya jamii na taifa kwa ujumla,” alisema.

Alisema hamasa ya kujiunga na mafunzo hayo ni ndogo   huku fursa nyingi zimekuwa zikichukuliwa na watu kutoka mikoa mbalimbali ambayo haina vyuo vya ufundi.

Juma Ally ambaye ni mkazi wa Wilaya ya Maswa, alisema   vyuo hivyo vikitumiwa vizuri vitasaidia kupunguza idadi ya vijana kuajiriwa kwa vile  wanaweza kujiajiri  wenyewe.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles