31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Serikali yagoma kutoa tenda miradi ya maji kwa wakandarasi

Amina Omari, Tanga

Serikali imesema haitatoa usimamizi wa miradi ya maji kwa wakandarasi badala yake itazitumia mamlaka zake za maji ili kuhatakisha upatikanaji wa huduma hiyo kwa wananchi.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa, wakati akipokea taarifa za sekta ya maji kuitoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigela wakati wa ziara yake mkoani hapo.

Amesema kufanya hivyo kutasaidia kuzijengea uwezo mamlaka hizo katika utekelezaji wa miradi pamoja na kupunguza gharama za utekelezaji wa miradi hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Tanga aliiomba serikali kuwasaidia kutafuta ufumbuzi wa kero ya huduma ya maji katika wilaya za Muheza, Pangani na Mkinga.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles