30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Serikali yagawa hati 250 za matumizi bora ya ardhi Korogwe

Amina Omari, Korogwe

Serikali imegawa hati 250 za kimila za matumizi bora ya ardhi kwa wilaya ya Korogwe ili kudhibiti uharibifu wa vyanzo vya maji.

Akikabidhi hati hizo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigela Mkuu wa Wilaya ya Muheza Mwanasha Tumbo amesema kuwa ugawaji wa hati hizo umelenga katika kuhakikisha wanadhibiti uharibifu wa mazingira pamoja na kupunguza migogoro ya ardhi.

“Maji ni rasilimali muhimu hivyo ni lazima tuweke mipango endelevu ya kuhakikisha rasilimali hiyo inadumu kwa muda mrefu,” amesema.

Aidha mwakilishi mkazi wa UNDP Christine Musisi amesema kuwa uwepo wa hati hizo utaweza kusaidia kumaliza migogoro ya ardhi pamoja na kurasimisha makazi Bora kwa wananchi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles