27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

SERIKALI KUAJIRI WALIMU 10,140

Gabriel Mushi, Dodoma

Serikali inatarajia kuajiri walimu 10,140 katika shule za msingi ili kupunguza tatizo la uhaba wa walimu nchini.

Kauli hiyo imetolewa leo Mei 2, bungeni jijini Dodoma na Naibu wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Joseph Kakunda wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Ludewa, Deo Ngalawa (CCM).

Ngalawa alitaka kujua ni lini serikali itaanza kuajiri walimu katika jimbo lake ambalo linalokabiliwa na uhaba wa walimu hususani katika shule za msingi.

Akijibu swali hilo Kakunda amesema kwa sasa serikali inaendelea na ukaguzi wa vyeti vya walimu 10,140 ili waajiriwe kuanzia Juni 30 mwaka huu.

Aidha, amewataka wabunge kuvuta subira wakati serikali inakamilisha taratibu za ukaguzi wa vyeti hivyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles