23.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Sekta binafsi yazidi kuathiriwa

Godfrey Simbeye
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Godfrey Simbeye

Na Kulwa Mzee, Dar es Salaam

SEKTA binafsi inazidi kuathiriwa na sera za uwekezaji katika ngazi ya Taifa.

Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam hivi karibuni na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Godfrey Simbeye, wakati wa akifunga mkutano uliojadili mpango wa mazingira ya kuimarisha biashara Tanzania ulioandaliwa na Taasisi ya BEST-AC.

Alisema wamedhamiria kuhakikisha kuna mazingira mazuri ya biashara kwa umma na lazima yawe endelevu bila kujali kiwango cha maendeleo katika nchi.

“BEST AC imekuwa ikiendesha shughuli zake nchini kwa miaka 10 sasa na ninakiri kwamba pale tulipo hivi sasa si kama ilivyokuwa mwanzo,” alisema Sembeye.

Alisema BEST-AC imekuwa endelevu sehemu kubwa katika programu zake na mradi huo umeleta manufaa makubwa katika sekta binafsi na kufanya kuwepo kwa mwingiliano endelevu wa mafunzo kwa pande zote.

Alipongeza uamuzi uliotolewa na Serikali wa kufanya mazingira ya biashara kwa Taifa kama matokeo muhimu.

Alisema TPSF ilikuwa na wasiwasi suala la urasimu halijawahi kujadiliwa katika mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) kwa mazingira ya biashara.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa President’s Delivery Bureau (PDB), Peniel Lyimo, alipongeza BEST-AC kwa jukumu lake la kusaidia sekta binafsi kwa ajili ya kutetea mazingira bora ya biashara.

“BEST-AC wamefanya kazi nzuri na mchango wao ni mkubwa sana katika sekta hiyo,” alisema Lyimo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles