26.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

SABABU ZA KUTUMBULIWA JOKATE ZATAJWA

Na Mwandishi Wetu

Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Shaka Hamdu Shaka amesema kutenguliwa kwa uteuzi wa Kaimu Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi jumuiya hiyo, Jokate Mwegelo ni maazimio yaliyoridhiwa na Baraza Kuu la Jumuiya hiyo.

Uamuzi wa kutenguliwa kwa uteuzi huo wa Jokate, umetangazwa leo na Mwenyekiti wa UVCCM, Kheri James mjini Dodoma leo Jumapili Machi 25, Kufunga Kikao cha Baraza Kuu la jumuiya hiyo, iliyotanguliwa na semina elekezi huku akisisitiza nafasi hiyo itajazwa baadaye.

Akizungumza na Mtanzania Digital, Shaka amesema sababu za kutenguliwa kwa Jokate inatokana na uamuzi wa Kamati ya Utekelezaji ya Umoja huo iliyokutana kwa dharura leo mchana chini ya Mwenyekiti wake, Kheri na kuazimia kwa pamoja ambapo hatua hiyo ni utaratibu wa kawaida wa vikao vya baraza hilo ambapo ajenda inapowasilishwa bila kujali aliyewasilisha ni nani na kikao kinaporidhia inakuwa ni ajenda ya kikao.

“Itoshe tu kusema ni utaratibu wa kawaida ndani ya CCM pamoja na jumuiya zake kufanya mabadiliko ya aina yoyote pale wanapoona inafaa,” amesema shaka kwa kifupi.

Jokate ametumikia nafasi hiyo kwa miezi 11 tangu ateuliwe Aprili 24, mwaka jana.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles