LOS ANGELES, MAREKANI
NYOTA wa muziki wa Pop nchini Marekani, Robyn Fenty ‘Rihanna’, amekanusha taarifa zinazosambaa kwamba ana ujauzito.
Wiki chache zilizopita kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kulikuwa na taarifa kwamba mrembo huyo ana ujauzito kutokana na mwili wake kuwa mkubwa na kuongezeka uzito, lakini amekanusha.
“Ni kweli mwili wangu umekuwa mkubwa siku hizi na kilo zimeongezeka, lakini haimaanishi kama nina ujauzito.
“Hakuna siri kwenye ujauzito, nadhani kila kitu kitakuwa wazi endapo nitakuwa na ujauzito kwa kuwa sitaweza kujificha labda niwe nakaa ndani hadi najifungua,” alisema Rihanna.