28.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

Rebecca Malope kunogesha Tamasha la Pasaka

Rebecca MalopeNa Mwandishi Wetu

RAIA wa Afrika Kusini ambaye ni mwanamuziki wa injili, Rebecca Malope, amethibitisha kuwa mmoja wa waimbaji wa kimataifa watakaotumbuiza kwenye Tamasha la Pasaka litakalofanyika nchini.

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama, sambamba na Malope, Afrika Kusini wanatarajia kutoka waimbaji wengine wawili ambao ni Solly Mahlangu na Sipho Makabane.

Msama alisema waimbaji wengine waliokubali kutumbuiza kwenye tamasha hilo ni pamoja na Ephraim Sekeleti, Solomon Mukubwa, Upendo Nkone na Bonny Mwaitege,

Naye mjumbe wa kamati ya maandalizi, Khamis Pembe, alisema wako katika mipango mikubwa ya kufanikisha miaka 15 ya tamasha hilo ambalo litaongeza ukaribu na jamii yenye uhitaji maalumu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles