25.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

RC aahidi kusimamia ujenzi minara ya simu Tanga

Amina Omari, Tanga

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela amewahakikishia wananchi wa kata ya Magoroto wilayani Muheza upatikanaji mzuri huduma za mawasiliano kwa kusimamia ujenzi wa minara ya simu.

Ametoa ahadi hiyo leo Jumatatu Agosti 19, wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za maendeleo katika kata hiyo.

Amesema kuwa serikali ina mfuko wa mawasiliano hivyo atawasilisha kilio chao ili waweze kupeleka huduma hiyo katika wilaya hiyo.

“Tunajua huduma ya mawasiliano ni muhimu hivyo nitaleta wataalamu ambao wataweza kutembelea maeneo ambayo yataweza kuweka miundombinu ya minara na kuweza kupata huduma kwenye Kata hii. 

Mmoja wa wananchi hao John Rafael amesema kuwa kata hiyo haina huduma ya mawasiliano toka ilipoanzishwa jambo ambalo limekuwa ni kero kubwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles