27.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Polisi Tabora wanasa wanne wakiwa na SMG

Bunduki aina ya AK 47
Bunduki aina ya AK 47

NA VIVIAN SHANGO

JESHI la Polisi mkoani Tabora limewakamata watu wanne wakiwa na bunduki ya SMG ikiwa na risasi mbili, baada ya kuvamia Kijiji cha Tura wilayani Uyui.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Suzan Kaganda, alisema watuhumiwa hao walikamatwa baada ya kupigwa na wananchi ambao walimuua mtuhumiwa mmoja.

“Watu hawa wakiwa watano walivamia kijijini hapo, wakavunja na kupora Sh milioni 2.3.

“Lakini wakati wanataka kukimbia wakiwa na pikipiki walizungukwa na wananchi waliowashambulia na mmoja alipoteza maisha,” alisema Kamanda.

Kaganda alisema pia kuwa polisi waliwakamata Malimatamu Ndawayake (38), Shija Mihayo(40) na Mwinyimzee Kiloge (36) wakazi wa Wilaya ya Nzega, kwa kupatikana na magunia mawili na nusu ya bangi.

Katika operesheni hiyo watuhumiwa wengine sita walikamatwa wakiwa na lita 160 za gongo.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Achimwene Peter (45), Hamisi Songambele (45), Sofia Stepheno (42)Thadeo Paulo (37), Devotha Paulo (26) na Aziza Juma (35).

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles