MCHEZAJI wa timu ya Chelsea, Oscar dos Santos, amekana katika ukurasa wake wa Twitter kuhusika katika mzozo wa maneno yaliyojaa hasira na kutaka kupigana dhidi ya Diego Costa walipokuwa katika uwanja wa mazoezi Alhamisi iliyopita.
Moja ya sababu inayodaiwa kuwa ni chanzo cha ugomvi huo ni baada ya Oscar kumfanyia rafu Muhispania huyo na baadaye Costa kutaka kumrudishia ambapo hali hiyo ilisababishwa kutengwa katika uwanja wa mazoezi wa Cobham.
Hali hiyo ilibidi kuwazuia mara kwa mara kwa kutaka kukabiliana wakati wa mazoezi makali yaliyokuwa yakiendelea kwenye timu hiyo.