27.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Ommy Dimpoz kuwapenda wanaomchukia

dimpozNA JENNIFER ULLEMBO, DAR ES SALAAM
MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’, amesema hakuna haja ya kuwajengea chuki watu wanaojifanya kukupenda lakini hawafurahishwi na mafanikio yako.
Akizungumza na MTANZANIA hivi karibuni, Dimpoz ambaye alishindwa kufanya shoo nchini Marekani kutokana na visa yake kuwa na mapungufu, alisema imekuwa ni jambo la kawaida wasanii kuchukiwa bila sababu za msingi.
“Unajua mara nyingi unapoamua kuweka chuki sababu ya watu fulani ambao wamekuwa wakikuchekea ila ukweli hawafurahishwi na mafanikio yako ni kujiumiza bure,” alisema Ommy Dimpoz.
Alisema kwa sasa ameamua kufanya vitu vinavyomridhisha na kumpa furaha hata kama wengine watamfikiria vibaya na kumsema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles