24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Ofisa wa JWTZ kizimbani kwa kubaka watoto watatu

Walter Mguluchuma -Katavi

OFISA mstaafu wa  Jeshi la  Wananchi wa Tanzania ambaye alistaafu hivi karibuni akiwa na cheo cha Meja, Inginus Isanga  (54) amekikishwa katika Mahakama ya Hakimu  Mkazi Katavi  kwa tuhuma za kuwabaka watoto watatu Wanafunzi wa darasa la tatu na la nne wa shule ya Msingi  Muungano katika Manispaa ya Mpanda.

Watoto hao, wawili ni wa familia moja.

Mtuhumiwa huyo alifikishwa mahakamani jana kusomewa na mashitaka na Mwendesha Mashtaka Mfawidhi  wa ofisi  ya Taifa  ya mashitaka  Mkoa wa Katavi,  Elisante  Masaki mbele ya  Hakimu  Mkazi Mfawidhi  wa Mahakama  ya Hakimu Mkazi Katavi, Emanuel  Ngigwana.

Mwendesha mashitaka huyo alidai kuwa mtuhumiwa huyo ambae ni ofisa mstaafu wa JWTZ alitenda kosa hilo la kuwabaka watoto hao kwa nyakati tofauti kati ya Machi 1 na 2 mwaka huu.

Alidai  mtuhumiwa aliwatongoza watoto hao wenye umri wa miaka 13 na 14 ambao ni wanafunzi wanaosoma katika shule ya Msingi Muungano katika Manispaa ya Mpanda   darasa la tatu na la nne kwa kuwaahidi kuwapatia kiasi cha Sh 20,000 kila mmoja.

Mwendesha mashitaka huyo alidai kuwa mshitakiwa aliweza kuwabaka watoto hao katika nyakati tofauti katika nyumba ya kulala wageni iliyoko katika Mtaa wa Tambukaleli na kuwapatia kiasi cha Tshs 20,000 baada ya kuwa amewafanyia kitendo hicho cha kuwabaka .

Baada ya mshitakiwa kusomewa mashataka hayo, Hakimu  Ngigwana  alitaka ayajibu kama   anayakubali au anayakataa ili mahakama iweze kuendelea na taratibu nyingine za kesi hiyo .

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles